POLE POLE AJIUZULU, ASEMA UONGOZI HAUTENDI HAKI


Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, amemuandikia barua Rais Samia akitangaza kujiuzulu nafasi ya uwakilishi wa Tanzania nchini Cuba, eneo la Karibe, Amerika ya Kati pamoja na nchi rafiki za Colombia, Venezuela na Guyana
Katika barua hiyo, Polepole ameeleza kuwa ameamua kujiuzulu kutokana na mwelekeo wa kiuongozi unaokosa msimamo thabiti katika kusimamia haki za watu, amani, na heshima kwa wananchi
Aidha, ameeleza kutoridhishwa na kufifia kwa dhamira ya kweli ya uwajibikaji na kushughulikia changamoto za wananchi, sambamba na kudorora kwa maadili ya uongozi
Amesisitiza hawezi kuendelea kuwa sehemu ya uongozi usiohamasika na utii wa misingi ya katiba ya nchi na chama, haki, maadili, utu na uwajibikaji kwa wananchi
Polepole aliwahi kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Novemba 2020 – Machi 2022), Balozi Malawi (Machi 2022 – Aprili 2023) na Cuba (Aprili 2023 – Julai 2025)


 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Popular Items